Featured
Loading...

MWILI WA ASILI CHANZO CHA UTUMWA WA DHAMBI!

HAPA CHINI==>> >

Image result for sin
 MWILI WA ASILI CHANZO CHA UTUMWA WA
DHAMBI!
__________________________
Amani ya Bwana iwe nanyi wapendwa!
Kama kilivyo kichwa cha habari hapo
juu,tuchangie kuangalia mojawapo ya sifa za
mwili wa asili ambacho ndicho chanzo cha
utumwa wa dhambi!
Paulo asema:«Ndivyo ilivyoandikwa, Mtu wa
kwanza, Adamu, akawa nafsi iliyo hai; Adamu
wa mwisho ni roho yenye kuhuisha.Lakini
hautangulii ule wa roho, bali ule wa asili;
baadaye huja ule wa roho.Mtu wa kwanza
atoka katika nchi, ni wa udongo. Mtu wa pili
atoka mbinguni.Kama alivyo yeye wa udongo,
ndivyo walivyo walio wa udongo; na kama
alivyo yeye wa mbinguni, ndivyo walivyo walio
wa mbinguni.Na kama tulivyoichukua sura
yake yule wa udongo, kadhalika tutaichukua
sura yake yeye aliye wa mbinguni.»1Kori
ntho15:45-49
Kakika mafungu haya tunaona akina Adamu
wa wili(Adamu wa Edeni na Adamu wa
mbingu)
*Adamu wa Edeni ni wa udongo,
*Adamu wa Mbinguni ni wa Roho,
★Anasema kuwa wote kwa kuazliwa
tulichukuwa asili ya baba yetu wa dunia,ila
kwa neema ya damu ya Yesu twaweza kuingia
katika muunganiko wa kuchukua asili ya
Adamu wa mbinguni!
Wapendwa baada ya dhambi kuingia
ulimwenguni,mwanadamu alijiunga na adui
wa Mungu kupinga makusudi ya mbingu,na
kadri alivyo kuwa na kuimarika katika asili
hiyo,aliendelea kuwa mbali na Mungu na
kuvumbua uasi mpya!!
Soma hapa:«Baada ya dhambi,sheteni
hakupumzika aliazimia atakao waangusha
kama yy alivyoanguka.Kama alivyowadangany
a malaika ili wamgomee Mungu ndivyo
alivyomshawishi Adamu(wa udongo) kukiuka
(violer) sheria ya Mungu.Hivyo Adamu akaasi
kama Lucifer.Zaidi ya hayo Shetani na Adamu
wakawa marafiki,na wakajipanga kushambulia
mbingu kwa pamoja!»GC chap30 uk503
Nasi tukazaliwa na huyo huyo na kwa asili
tukawa tu maadui wa mapenzi ya Mungu na
tukawa hatuna nguvu ya kutenda mema na
ndiyo sababu mnaona huwa :udokozi,wizi,k
utukana,kukasirika,kulipiza kisasi,kuzini,nk
hayo hayafundishwi bali ni asili ya kila
mwanadamu!!!!!!
Paulo asema:«Kwa hiyo, kama kwa mtu
mmoja dhambi iliingia ulimwenguni, na kwa
dhambi hiyo mauti; na hivyo mauti ikawafikia
watu wote kwa sababu wote wamefanya
dhambi»Rumi5:12
Kwa sababu hizo ndani yetu kupitia Adamu
tulipoteza uwezo wa kutii sheria ya Mungu,
(Rumi8:7) na hicho ndicho chanzo cha wengi
hawawezi kutulia ndani ya Haki ya Mungu!
Yesu alisema:«Yesu akawajibu, Amin, amin,
nawaambia, Kila atendaye dhambi ni mtumwa
wa dhambi.Wala mtumwa hakai nyumbani
sikuzote; mwana hukaa sikuzote.Basi Mwana
akiwaweka huru, mtakuwa huru kweli
kweli»Yohana8:34-
Hiyo ndiyo sababu unaona wengi hujidai_,oh
mimi ni mtumishi,oh mimi nineokoka
oh...kama mafarisayo walivyomjibu
Yesu,wakisema kuwa wao si watumwa wa
mtu,kwa usemi mwingine walimwambia sisi
tumeokoka Yesu, # swali la kujiuliza ni“mimi
nimtumwa au niko huru?”
# Kuwa huru nje ya dhambi,siyo kuwa:
*mhubiri,*mchungaji,*

mwinjilisti,*mzee wa
kanisa nk ni zaidi ya hayo!!
Maana mmekuwa mkishuhudia ninyi wenyewe
wenye vyeo hivyo lakini,wakiwa bado
wanalawiti wafanyakazi wao,kutembea nje ya
ndoa,wengine kupata ukimwi nje ya
ndoa,kusuka nywele,kuklimu,vimini,suluale
kwa wana-mama nk(Je kweli hawa
wameokoka?)
WAPI NIPATE MSAADA WA KUNIPONYA?
____________________________
Paul alipokuwa bado ni mtumwa aliguswa na
hali ya Kimungu hivyo akalia akisema:«Ole
wangu, maskini mimi! Ni nani atakayeniokoa
na mwili huu wa mauti?»Rumi7:24
Yesu alijibu na kuwaita wote waliojikuta ktk
hali hiyo akisema:"Njooni kwangu ninyi
nyote»Mathayo11:28
Hapa aliahidi kukupa nguvu na uwezo,uwezo
ule ulioupoteza ktk Adamu wa udongo
utaupokea ktk Adamu wa Roho kwa njia ya
imani!
Yesu asema:«Bali wote waliompokea aliwapa
uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio
wale waliaminio jina lake»Yoh1:12
Ombi:Katika jina la Yedu na kupitia damu
yenye nguvu ya Kalvary,pokea nguvu,na uwezo
ili kushinda mwili wa asili,Kristo aanzishe vita
ndani yako akishindana na utu wa kale,ili
akupe nguvu za kuishi utu upya na kudumu
ktk Uhuru nje ya Dhambi»
Ninyi mmekuwa rafiki zangu, mkitenda
niwaamuruyo»Yoh15 :14
(CLICK HERE)==>>>

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright JIFUNZE MAANDIKO | Designed By Tandy boy
Back To Top